Thursday, February 28, 2013

ILIKUWA LAZIMA WAFELI

ILIKUWA LAZIMA WAFELI Stori: Mwandishi Wetu MBALI na mfumo mbaya wa elimu unaolalamikiwa na wadau nchini kwamba umechangia matokeo mab... thumbnail 1 summary

ILIKUWA LAZIMA WAFELI

Stori: Mwandishi Wetu
MBALI na mfumo mbaya wa elimu unaolalamikiwa na wadau nchini kwamba umechangia matokeo mabaya ya kidato cha nne, lakini vitendo wanavyovifanya wanafunzi wakiwa shuleni pia vina mchango wa matokeo mabaya, Amani limechimbua.
Mitandao mbalimbali ya Bongo, imerusha picha kadhaa zikiwaonesha wanafunzi wakiwa katika vitendo vinavyoashiria ufuska, usagaji na ngono. Amani lilipata bahati ya kuzungumza na wadau, walimu na wazazi ambapo baadhi yao walikiri kuwa kuna wanafunzi wanaoendekeza vitendo vichafu wakiwa shuleni hali inayosababisha kufanya vibaya katika mitihani.
“We fi kiria, mwanafunzi wa kike anakwenda shuleni akiwa na simu yenye intaneti, anaona matukio machafu ya duniani, huyu anaweza kuzingatia masomo kweli? “Mbaya zaidi, vitendo wanavyoviona kwenye mitandao na wao huviiga kwa kuvifanya wenyewe kwa wenyewe,” alisema Bakari Mzuri, mkazi wa Magomeni, Dar es Salaam.
Ikazidi kuelezwa kwamba asilimia kubwa ya wanafunzi wa kike wana uhusiano wa kimapenzi na wanafunzi wa kiume au watu wazima wa mitaani.
Pia imebainika kuwa wapo wanafunzi, hasa wa vyuo, wanapofunga shule badala ya kurudi kwa wazazi wao kusaidia majukumu ya
kifamilia wanakwenda kuishi na wapenzi wao sehemu nyingine huku wakidanganya makwao kwamba wametakiwa kubaki zamu.
Matokeo ya mitihani ya kidato cha nne mwaka 2012 yanaonesha hivi:
Divisheni 0 ni 240,903 (60.1%), divisheni IV ni 103,327 (26%), divisheni III ni 15,426 (3.9%), divisheni II ni 6,433 (1.6%) na divisheni I ni 1,641 (0.49%).
Wakati huohuo, wazazi nchini wamelalamikia matumizi tofauti ya vitabu vya masomo wakisema pia yanachangia matokeo
mabaya ya mitihani.
Walitoa mfano kwa kusema kuwa, utakuta kitabu cha hesabu darasa la nne shule ya msingi ya serikali siyo kinachotumika
shule za msingi za binafsi, hali inayosababisha uelewa tofauti wa wanafunzi.

Saturday, February 23, 2013

TANZANIA YATINGA KWENYE KUMI BORA NDANI YA LONDON FASHION WEEK.‏

TANZANIA YATINGA KWENYE KUMI BORA NDANI YA LONDON FASHION WEEK.‏ Wabunifu miti... thumbnail 1 summary

TANZANIA YATINGA KWENYE KUMI BORA NDANI YA LONDON FASHION WEEK.‏

Wabunifu mitindo Jackline Kibacha na Anna Lukindo wakisindikizwa na Mama Balozi Joyce Kallanghe na Mama Rose Kiondo

Nje ya Jumba la Somerset…
Wabunifu mitindo Jackline Kibacha na Anna Lukindo wakisindikizwa na Mama Balozi Joyce Kallanghe na Mama Rose Kiondo
Nje ya Jumba la Somerset
Wanamitindo wa Kitanzania kwenye London Fashion Week 2013. Anna Lukindo, Christine Mhando, Jacquline Kibacha
Mama Rose Kiondo, Samson Soboye, Mama Joyce Kallaghe, Anna Lukindo, Christine Mhando, Jacquline Kibacha
Barabara ya The Strand
Anna Luks
London Fashion Week 2013
Jumapili mchana  wilaya ya Westminster jijini  London ilikuwa na mashindano ya ubunifu na urembo katika maonyesho  ya kimataifa ya London Fashion Week. Mashindano haya yalifanyika jumba la Somerset lililosimama imara  kwenye upembe wa  kaskazi ya mto Thames.
Maonyesho ya London Fashion Week, bado yanaendelea jumba hili  la Somerset toka tarehe 14 hadi tarehe 28. Wiki hizi mbili nzima zitakutanisha kila mtu anaye husika na biashara ya mavazi na urembo. Magwiji na mapapa wa mitindo, wabunifu, walimbwende, watafuta vipaji, wafanya biashara, wazalishaji mali ghafi na wamiliki viwanda.  Wote hukutana katika maonyesho haya. Hapa si vipaji tu vinavyojionyesha, bali pia watu wa biashara.

Siku hii Tanzania ilikuwa moja ya nchi mbili tu za Kiafrika zilizochaguliwa na British Council na LFW kushiriki kwenye mashindano  ya kutafuta vipaji chipukizi kwenye tasnia ya ubunifu wa mavazi na urembo.  Watanzania Anna Lukindo, Jacqueline Kibacha na  Christine Mhando ndio wasanii waliobeba bendera ya taifa letu na kutuwakilisha katika mashindano haya ya kimataifa yanayofanyika kila mwaka kwa zaidi ya miaka 27 sasa.

Katika kuunga mkono maendeleo ya Tanzania na Watanzania,  Ubalozi wetu  Uingereza na Bodi ya Utalii Tanzania, nao pia walichukua nafasi hii kuwasaidia wananchi hawa kufanikisha mahitaji yao ya ushindani. Ubalozi umetoa Ukumbi wa Nyumba Ya Tanzania ulioko Bond Street ili wasanii hao waweze kuonyesha nguo na sanaa zao kwa juma zima kama sheria za London Fashion Week zinavyoamuru. Vile vile Bodi ya Utalii ya Tanzania imesaidia katika mchango  wa mali ghafi zilizotumika katika shughuli hizi  ili kuiuza Tanzania kimataifa.

Mshindi wa tukio alikua Estonia. Ingawa  Tanzania haikuwa mshindi wa mwanzo- ilichaguliwa kati ya Kumi Bora jambo ambalo limetikisa nyoyo na vichwa vya  waandaaji, wabunifu,wafanya biashara na watafuta vipaji vya kimataifa. Hii ni mara ya kwanza kwa taifa letu kushiriki katika shughuli na  wote wameguswa na kupumbazwa na usanii wa hali ya juu ulioonyeshwa na wasanii  watatu wa Kitanzania.   Lukindo, Mhando na Kibacha wamechukua nafasi waliyopewa kwa mikono miwili na wote wameisogeza Tanzania hatua moja zaidi ndani ya ulingo wa kimataifa na katika biashara hii ya mavazi na urembo ambayo inasemekana ina thamani ya  Pauni Billioni 10  ama  shilingi Trillion 25 za Tanzania.

Thursday, February 21, 2013

Q-CHIEF AMJIBU DIAMOND, ‘HE IS A GOOD KID, I LOVE HIS MUSIC, SIAMINI KATIKA UCHAWI’

Baada ya jana Diamond Platnumz kufunguka kwa undani jinsi anavyochukizwa na kitendo cha mwanamuziki mwenzie Abubakar Katwila aka Q-Chief ... thumbnail 1 summary
Baada ya jana Diamond Platnumz kufunguka kwa undani jinsi anavyochukizwa na kitendo cha mwanamuziki mwenzie Abubakar Katwila aka Q-Chief kumsema anatembelea nyota yake, Q-Chief amezungumza na Bongo5 kujibu shutuma hizo.
Katika kipindi cha XXL cha Clouds FM jana, Diamond alisema, “mimi sipendezewi na anvyowaambia watu kuwa mimi namroga, kwa nini nisitembelee nyota ya watu kama akina Omary, akina Ben Pol. Alumbane na wakubwa wenzie akina Dully Sykes, mimi sitaki, namheshimu abishane na wakubwa wenzie, mimi mdogo aniache na wadogo wenzangu.”
Akijibu shutuma hizo, Q-Chief amesema:
“Sijui wakati anajibu hayo maswali alikuwa kwenye hali gani, sijui alikuwa amekasirika, sijui alikuwa 'out of mood' sijui alikuwa okay, lakini 'all in all' najua kila mtu ana uhuru wa kuongea kile anachojisikia na hajawekea mipaka, as long as kina-msatisfy yeye na kinawafurahisha wengine kwenye umma.
Mimi watu wangu wamenichukulia positive hili jambo baada ya kusikikiliza walinirekodia nikasikiliza lakini 'am not a big fan of superstition so' siamini hivyo vitu lakini kitu ambacho naweza kusema huu najua ni mchezo mchafu na acha niucheze kwa hisia kwa sababu sijui huko mbele ni kitu gani kitakuja kunisaidia katika maisha na kunyamaza pia wakubwa wanasema ni ustaarabu. He is a good kid, I love his music, he is doing good.”
Pia Q-Chief ambaye wiki iliyopita aliachia wimbo mpya uitwa Akuro amesema atafurahi kumuona Diamond anakuja kwenye show yake ya kwanza tangu miaka mitano iliyopita itakayofanyika kwenye ukumbi wa New Maisha Club, Jumapili ya Februari 24.
“Ningependa awepo kwenye hii show aangalie kwa sababu mimi pia nimekuwa nikihudhuria na nimeshawahi kufanya show ya Diamonds are Forever naye aliniita kwa mapenzi yake and with open-hearted I did a good show,” amesema Q.

RAIS WA KENYA AZINDUA BARABARA YA MWAI KIBAKI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

RAIS WA KENYA AZINDUA BARABARA YA MWAI KIBAKI JIJINI DAR ES SALAAM LEO ... thumbnail 1 summary

RAIS WA KENYA AZINDUA BARABARA YA MWAI KIBAKI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais Mwai Kibaki wa Kenya wakiongozwa na Meya wa Kinondoni Mstahiki Yusuph  Mwenda kutembea hatua chache kabla ya kuzindua rasmi jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jina la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013.

Rais Mwai Kibaki wa Kenya akikata utepe, akishuhudiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri…
Rais Jakaya Mrisho Kikwete na mgeni wake Rais Mwai Kibaki wa Kenya wakiongozwa na Meya wa Kinondoni Mstahiki Yusuph  Mwenda kutembea hatua chache kabla ya kuzindua rasmi jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jina la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013.
Rais Mwai Kibaki wa Kenya akikata utepe, akishuhudiwa na mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete, Waziri wa Ujenzi Dkt John Pombe Magufuli na Meya wa Kinondoni Mstahiki Yusuph Mwenda kuzindua rasmi  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jina la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo.
Bendi ya Vijana Jazz ikitumbuiza wakati wa uzinduzi rasmi  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013.
Sehemu ya barabara iliyopewa  rasmi  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jiba la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo leo Februari 21, 2013.
Meya wa Kinondoni Mstahiki Yusuph Mwenda akimkabidhi zawadi ya kasha la Zanzibar Rais Mwai Kibaki huku  mwenyeji wake Rais Jakaya Mrisho Kikwete akishuhudia katika uzinduzi  rasmi wa  jina la Barabara ya Mwai Kibaki linalochukua nafasi ya jina la barabara ya Old Bagamoyo leo kwenye makutano ya barabara ya Bagamoyo na Rashid Kawawa na iliyokuwa Old Bagamoyo.
(PICHA NA IKULU)

Monday, February 18, 2013

TUELIMIKE KUHUSU WIVU ILI TUSHEREHEKEE VALENTINE’S DAY VIZURI - 3 ... thumbnail 1 summary


TUELIMIKE KUHUSU WIVU ILI TUSHEREHEKEE VALENTINE’S DAY VIZURI - 3


TUNAENDELEA na mada yetu tuliyoianza wiki mbili zilizopita kuhusu namna ya kukabiliana na wivu. Endelea...

Kwa mawazo yake, tabia yako ya kutojiamini, hufikiria kwamba hakupendi.
Ikitokea akawa anafanya mawasiliano na mtu wa jinsia kama yako, hapo unaanza kuweweseka, mara ukasirike, upekue simu yake bila sababu, umkaripie, unune na kususa kuzungumza naye. Hiyo ni kujipa jakamoyo. Unashindwa kujiamini kama wewe ni zaidi ya huyo anayewasiliana naye. Unaogopa atakupora mpenzi.

Kwa mwanamke, kama anamhofia mwenzi wake…
TUNAENDELEA na mada yetu tuliyoianza wiki mbili zilizopita kuhusu namna ya kukabiliana na wivu. Endelea...
Kwa mawazo yake, tabia yako ya kutojiamini, hufikiria kwamba hakupendi.
Ikitokea akawa anafanya mawasiliano na mtu wa jinsia kama yako, hapo unaanza kuweweseka, mara ukasirike, upekue simu yake bila sababu, umkaripie, unune na kususa kuzungumza naye. Hiyo ni kujipa jakamoyo. Unashindwa kujiamini kama wewe ni zaidi ya huyo anayewasiliana naye. Unaogopa atakupora mpenzi.
Kwa mwanamke, kama anamhofia mwenzi wake kwamba anaweza kumsaliti kwa kutoka na mtu ambaye huwa anawasiliana naye, hiyo ni sawa na kujiwashia taa nyekundu. Si ajabu kutokujiamini kwako kukamfanya mwezi wako aone bora amalize kesi moja kwa moja. Vilevile, kwa mwanamke mwenzako atavimba kichwa, kuona hujiamini kwa sababu yake.
Kwa mwanaume, itakufanya ukose sifa za kuonekana kidume. Mwenzi wako atakuona msumbufu na unamkosea heshima kumtuhumu kwamba anaweza kukusaliti. Amini kwamba wewe ni wa ukweli na mpenzi wako anatosheka kwa makali ambayo unayo.
Usipojiamini, utampa kichwa huyo unayemuogopa. Muamini kuwa hatakusaliti na endapo unadhani anaweza kukuendea kinyume, huna haja ya kuishi naye. Ni rahisi kuonekana katuni kwenye jamii, mjinga, bwege kama hujiamini.
Linda heshima yako, dhibiti wivu wako, jiamini. Hayo ni mambo ambayo yanaweza kukupa uwezo wa kukabili changamoto mbalimbali ambazo zinaweza kuusumbua moyo wako kwa kuupa wasiwasi kuwa mwenzi wako anakuendea ndivyo sivyo.
“Yule ndugu ananiogopa kweli, anahisi namchukua mtu wake,” hii kauli anaweza kuitamka huyo ambaye wewe huna imani naye. Tambua kuwa unampa kichwa kwa maana hata jinsi anavyozungumza anaashiria kuwa yeye ndiye amebeba amani yako. Usimfanye binadamu mwenzako akajiona hivyo.
6. WASILIANA MARA KWA MARA
Una wasiwasi na mahali ambako mwenzi wako yupo? Huna amani na unahisi anakusaliti? Moyo wako umefunikwa na jakamoyo na kila hatua mapigo yanaongezeka kasi au yanashuka? Kimsingi huna sababu ya kuwa hivyo. Usiishi kwa dhana, ila simamia vitu vinavyoonekana.
Mawasiliano ni njia bora kabisa ya kudhibiti wivu. Mnapozungumza mara kwa mara au ‘kuchati’ kwa SMS, Facebook au mitandao mingine ya kijamii, huwaweka karibu. Kama una hali ya wasiwasi, itakwisha au kupungua kwa sababu muda wote utajiona kama mpo pamoja.
Je, mkiwa wawili chumbani au sehemu yoyote ya faragha, bila simu wala mtu wa tatu anayeweza kuingilia ukaribu wenu, mnaweza kuanza kulumbana kwa sababu ya kuoneana wivu? Jibu ni hapana. Hivyo basi, mawasiliano ya mara kwa mara huwaweka karibu na ni salama zaidi kuliko hata mngekuwa wawili chumbani.
Mawasiliano yasiwe yenye kuishia katika simu au mitandao, kama hamjafunga ndoa au tayari ni wanandoa lakini hamuishi pamoja, jitahidini kukutana mara kwa mara. Ikiwa mnaishi eneo moja, wekeni utaratibu wa kuonana kila inapobidi, hiyo itasaidia kukuza upendo na amani ambayo itayeyusha hulka za wivu.
Wakati ukitekeleza hili la kuonana mara kwa mara na mwenzi wako, si vibaya ukamwambia jinsi unavyoumizwa na tabia ya yeye kufanya mawasiliano ya karibu na watu wenye jinsia tofauti na yeye. Ukizungumza naye kwa upole, hali itakuwa nzuri kuliko kulaumu au kulalamika.
Hoja ya wivu iwekwe mezani halafu muijadili kwa upana. Kitendo cha kujadili na mwenzi wako jinsi wivu unavyokutesa, kitasaidia kuweka mwanga na kupata ufumbuzi wa tatizo husika. Kama atajua mambo ambayo akiyafanya utaumia halafu akatekeleza bila woga, maana yake atakuwa amedhamiria kukuumiza, hivyo hakufai kwa maisha yako.
Kama usipomwambia ukweli, itakuwa ngumu kwa mwenzi wako kujua jinsi ya kukusaidia kuyakabili hayo maumivu unayoyapata kwa sababu ya wivu. Waungwana wanasema kuwa dirisha la mazungumzo, hurahisisha yabisi kuwa laini. Anza leo kuamini katika kumshirikisha mwenzi wako uone matunda yake.
Shika kanuni hii “zungumza sana, ubishi hapana”, utakuwa kituko endapo utajibiidisha na ubishi badala ya kuzungumza kwa lengo la kumpa muongozo. Wivu ni chachandu lakini ukizidi mapenzi huonekana tamu yenye uchungu.
Itaendelea wiki ijayo.

Sunday, February 17, 2013

LINEX: THE WAY NILIVYOKUA NAISHI ILIKUA INAFIKIA POINT WATOTO WA KIKE WANACHOKA MAISHA YANGU YA MTAANI SO WANAAMUA KUNIACHA

LINEX: THE WAY NILIVYOKUA NAISHI ILIKUA INAFIKIA POINT WATOTO WA KIKE WANACHOKA MAISHA YANGU YA MTAANI SO WANAAMUA KUNIACHA Linex akiwa... thumbnail 1 summary

LINEX: THE WAY NILIVYOKUA NAISHI ILIKUA INAFIKIA POINT WATOTO WA KIKE WANACHOKA MAISHA YANGU YA MTAANI SO WANAAMUA KUNIACHA


Linex akiwa na shemeji yetu "Suvi" kushoto

 Kama unakumbuka vizuri, miezi kadhaa iliyopita, baada ya kuandikwa kwenye  magazeti ya udaku kuwa anamsichana mwingine, na yeye kuruka futi mia na kusema bado yupo na mpenzi wake wa kizungu "Suvi" ambae ndio kila kitu kwake, leo hii Linex amethibitisha kuwa mambo yao hakuna anaeweza kuyaingilia..ukimsikiliza kwa makini utagundua kuwa anajiami sana kwa mpenzi wake huyo na ndo maana anajaribu kukuambia kuwa atakua ana matatizo kama kuna kvuvi atakae weza kutupa nyavu baharini na kumvua mpenzi wake wa sasa.

"kama kuna mvuvi atatupa nyavu kumvua huyu shemeji yenu wa sasa hivi basi ntakua nna tatizo, kwasababu maisha yangu mengi, nafkiri labda kwa sababu ya the way i was living, sababu unajua mi ntaokea mtaani sasa labda the way nilivyokuwa naishi ilikua inafikia point watoto wa kike wanachoka maisha yangu ya mtaani na nini,  so wanaamua kunichoka na wanaamua kuniacha na kuanza na maisha mengine, so hakuna jambo jipya kwenye swala la kupenda k wangu mimi yaani ...mi sina kinyongo na mvuvi ambae atatupa nyavu baharini atafanikisha kumvua samaki ambae mi nilikua napenda kumuona aendelee kuwa baharini akifanya maswala yeke".