Thursday, February 27, 2014

Ufaransa yazuia washukiwa kurudi Rwanda

Watutsi wengi waliuawa wakati wa mauaji ya Kimbari mwaka 1994 Mahaka... thumbnail 1 summary

Watutsi wengi waliuawa wakati wa mauaji ya Kimbari mwaka 1994
Mahakama nchini Ufaransa, imezuia mipango ya kuwarejesha nyumbani washukiwa watatu wa mauaji ya halaiki nchini Rwanda mwaka 1994, kuhukumiwa mjini Kigali.
Mahakama hiyo iliamua kuwa wanaume hao hawataweza kufunguliwa mashitaka nchini Rwanda, kwa kosa ambalo halikufafanuliwa kisheria wakati ambapo uhalifu huo ilitokea.
Mauaji ya kimbari yalianza kuwa kosa la kuadhibiwa nchini Rwanda chini ya sheria ambazo zilipitishwa kati ya mwaka 1996 hadi 2004.
Takriban watu 800,000 wengi wa kabila la Tutsi na wachache wa Hutu, waliuawa kwenye vita vya kikabila mwaka 1994.
Wapiganaji kutoka kabila la Hutu walituhumiwa kwa kufanya mauaji hayo.
Mahakama ilibatilisha uamuzi uliotolewa na mahakama ya Rufaa mwaka jana na kuidhinisha kuhamishwa kwa Claude Muhayimana na Innocent Musabyimana kukabiliana na kesi dhidi yao nchini Rwanda.
Pia ilisisitiza kusalia kwa hukumu ya mahakama iliyotolewa mwezi Septemba , ikakatalia mbali kuhamishwa kwa Laurent Serubuga nchini Rwamba.
Alikuwa naibu mkuu wa jeshi wa Rwanda wakati mauaji ya kimbari yalipofanyika.
Bwana Muhayimana, ni raia wa Rwanda na Ufaransa na anatuhumiwa kwa kushiriki mauaji ya Watutsi mjini Kibuye magharibi mwa Rwanda.
Naye Bwana Musabyimana anadaiwa kuhusika na mauaji katika mkoa wa Gisenyi.
Mwezi Julai mwaka jana Bwana Serubuga alizuiliwa nchini Ufaransa baada ya kutolewa kibali cha kumkamata na mahakama ya Rwanda.

Viktor Yanukovych aomba Urusi kumlinda

Viktor Yanukovych anasema angali Rais wa Ukraine Baada ya kutoweka m... thumbnail 1 summary

Viktor Yanukovych anasema angali Rais wa Ukraine
Baada ya kutoweka mwishoni mwa wiki, aliyekuwa Rais wa Ukraine Viktor Yanukoovich, anasemekana kuonekana nchini Urusi.
Hii ni kwa mujibu wa vyombo vya habari nchini Urusi ambavyo vimenukuu taarifa kutoka kwake.
Lakini bado hakuna taarifa kamili kuhusu aliko hasa.
Katika taarifa yake alisema kuwa bado yeye ni Rais wa Ukraine ingawa anaitaka serikali ya Urusi kuhakikisha usalama wake.
Taarifa hiyo, kutoka kwa Viktor Yanukovych ilitolewa na shirika rasmi la habari la Urusi na kusomwa kwenye televisheni nchini humo
Katika taarifa hiyo amesema kuwa yungali Rais wa Ukraine na anaamini kwamba vikao vya wabunge vinavyoendelea katika bunge la Ukraine sio halali.
Alisema kuwa ameitaka Urusi kumlinda kutoka kwa watu wenye siasa kali ambao walitwa mamlaka nchini Ukraine.
Aliongeza kuwa watu wa Kusini na Mashariki ya Ukraine na katika eneo la Crimea hawatakubali hali mbaya ya kisiasa ambapo mawaziri wa serikali wanaidhinishwa na makundi ya watu na kuonya dhidi ya kutokea vita vya wenyewe kwa wenyewe katika siku zijazo.
Alikanusha madai kuwa aliamuru wanajeshi kuingilia mzozo wa kisiasa nchini humo na kuwa hatafanya hivyo kamwe ila ataendelea kutafuta suluhu.

Mchezaji mkongwe Mario Coluna afariki

Mario Coluna Aliyekuwa nahodha wa timu ya soka ya Benfica kutoka ... thumbnail 1 summary

Mario Coluna
Aliyekuwa nahodha wa timu ya soka ya Benfica kutoka Msumbiji Mario Coluna amefariki nchini Msumbuji akiwa na umri wa miaka sabini na nane.
Coluna aliongoza timu ya Benfica kushinda mataji kadhaa barani ulaya na vile vile aliichezea timu ya taifa ya ureno katika fainali za kombe la dunia mwaka wa 1966.
Alipostaafu Coluna alirejea nyumbani ambako alichaguliwa kuwa mwenyekiti wa shirikisho la mchezo wa soka nchini Msumbiji.
Serikali ya Msumbiji imetangaza kua Coluna atapewa mazishi ya heshima zote za kitaifa.
Kifo chake kimetokea mwezi mmoja baada ya kifo cha mwanakandanda mwengine mashuhuri wa Msumbiji Eusebio aliyefariki nchini Ureno.

Real yailaza schalke 6-1

Ronaldo na Bale washerekea ushindi dhidi ya Schalke 04 Mchezaji b... thumbnail 1 summary

Ronaldo na Bale washerekea ushindi dhidi ya Schalke 04
Mchezaji bora duniani mwaka huu Cristiano Ronaldo Gareth Bale na Karim Benzima walifunga mabao mawili kila mmoja na kuisaidia Real Madrid ya uhispania kufuzu kwenye robo fainali ya kombe la mabingwa barani ulaya baada ya kuinyeshea Schalke 04 ya Ujerumani mabao 6-1 katika mkondo wa kwanza uliosakatwa huko Ujerumani.
Benzima ndiye aliyefungua kivuno hicho cha mabao baada ya nipe nikupe kunako dakika ya 13.
Mchezaji aliyeigharimu Madrid kitita kikubwa zaidi msimu huu Gareth Bale akafanya mambo kuwa mawili kwa nunge dakika saba baadaye .
Kuanzia hapo kampeini ya vigogo hao wa ligi ya uhispania kunyanyua taji lao la kumi barani Uropa ilikuwa mbioni
kufuzu kwa hatua ya robo fainali .
Ronaldo alimpangua Joel Matip kwa miondoko ya aina yake na kufunga la tatu akimwacha kipa wa Schalke Fahrmann asijue azibe wapi azue wapi.
Masaibu ya wenyeji hao yaliongezeka Karim Benzema alipofuma bao la nne .
Bale akaongezea bao la tano kisha nyota wa Ureno Ronaldo akafunga kiziba mkonga na kudidimiza kabisa mtumaini ya timu ya tatu ya Ujerumani baada ya mabingwa Bayern Munich na washindi wa pili Borussia Dortmund kusonga mbele katika hatua ya robo fainali ya mchuano huo msimu huu.
Uchungu uliwazidi mashabiki wa nyumbani na wachache waliosalia uwanjani walishuhudia bao la kukata na shoka la nyota wao Klaas-Jan Huntelaar .
Huntelaar aliyeichezea Madrid (2009) kwa mkopo alifuma mkwaju wa kipekee uliomwacha Iker Casillas ameduwaa.
Hata hivyo bao hilo la kufutia machozi la dakika ya mwisho ya mechi haitakuwa na faida mbali na kunusuru hadhi ya kocha Jens Keller Schalke itakapozuru bernabou baada ya majuma mawili kwa mkondo wa pili.
Fernando Torres asherekea bao lake
Katika mechi nyengine iliyosakatwa usiku wa jana huko Instabul,Uturuki ,matumaini ya pekee ya timu ya Uingereza kusonga mbele katika hatua ya robo fainali yalitegemea matokeo baina ya wenyeji Galatasaray na Chelsea .

Matokeo ya mkondo wa Kwanza

  • Barcelona 2-0 Man City
  • Paris St-Germain 4-0 Bayer Leverkusen
  • Atletico Madrid 1-0 AC Milan
  • Bayern Munich 2-0 Arsenal
  • Manchester United 0-2 Olympiakos
  • Borussia Dortmund 4-2 Zenit St Petersburg
  • Chelsea 1-1 Galatasaray
  • Real Madrid 6-1 Schalke
Kwa kila hali na mizani mechi hii ilitarajiwa kuwa ngumu kwa Galatasaray chini ya kocha wa zamani wa Manchester city Roberto Mancini ikiongozwa na aliyekuwa mshambulizi wa Chelsea Didier Drogba na Emmanuel Ebue zamani akiichezea Arsenal ilikuwa inakabiliana na The Blues chini ya Kocha Jose Mourinho .
Uwanjani mashabiki wa nyumbani walinyamazishwa na bao la dakika ya 9 ya kipindi cha kwanza iliyofungwa na Fernando Torres.
Roberto Mancini alilazimika kufanya badiliko la mapema ilikuzia kuabishwa na wimbi la mashabulizi ya vijana wa Mourinho .
Katika kipindi cha pili juhudi za Galatasaray kujinasua zilizaa matunda Aurelien Chedjou alifunga bao la kusawazisha baada ya kutumia vyema mpira wa kona uliomchanganya Peter Cech .
Bao hilo ndilo litakaloamua mshindi baina ya timu hizo mbili zitakapokutana katika mechi ya mkondo wa pili tarehe 18 mwezi Machi huko Stamford Bridge .

Marekani yaonya Urusi kutoivamia Ukraine

Marekani yaonya Urusi isiivamie Ukraine Marekani imeionya serikali y... thumbnail 1 summary

Marekani yaonya Urusi isiivamie Ukraine
Marekani imeionya serikali ya Moscow isithubutu kutumia nguvu za kijeshi dhidi ya Ukraine.
Hatua hii inawadia siku moja tu baada ya Urusi kuamuru kufanyika kwa mazoezi ya kijeshi yanayoshirikisha askari wapiganaji laki moja na nusu kwenye mpaka wake na Ukraine .
Kujitokeza kwa wanajeshi wa Urusi kwenye mpaka na Ukraine kumeimarisha uhasama ulioko kati ya Urusi na mataifa ya Magharibi.
Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Marekani, John Kerry amesema kuwa Urusi inapaswa kukubali ushauri ya kwamba mataifa ya kigeni yasiingile mambo ya ndani ya Ukraine.
Alisema kuwa kujiingiza kijeshi katika hali ilivyo nchini Ukraine kwa hivi sasa ni kosa kubwa.
Mawaziri wa ulinzi kutoka mataifa ya muungano wa NATO wametoa taarifa ambapo wamesema kuwa wanachama wake wataendelea kuunga mkono uhuru na hadhi ya taifa la Ukraine.
Serikali ya Marekani imesema kuwa imetenga mbinu mbalimbali inazotazamia kutumia kuimarisha Ukraine kiuchumi, huku kukiendelea kuwa na hofu kuwa huenda taifa hilo likashindwa kuendelea kulipa madeni yake.
Kwa wakati huu msaada wa kijeshi pekee kwa Ukraine hautoshi kwani taifa linalotaka kusaidia lazima kwanza liimarishe hali ya kukubaliwa kwake katika taifa hili ambalo limegawanyika kwa imani yake kati ya Urusi na mataifa ya Magharibi.
Wabunge kadhaa wa Marekani wameonya kuwa Jumuiya ya Ulaya na Marekani wasipotoa msaada wa pesa taslimu Urusi huenda ikafanya hivyo.

Mourinho: Alalama kurekodiwa kwa siri

Jose Mourinho kocha wa Chelsea Kocha wa timu ya Chelsea ya England,... thumbnail 1 summary

Jose Mourinho kocha wa Chelsea
Kocha wa timu ya Chelsea ya England, Jose Mourinho ameshutumu tabia ya kurekodi kwa siri mazungumzo yake kuhusu wachezaji wa timu hiyo.
Mourinho amesema lilikuwa jambo la aibu kuona kwamba mazungumzo binafsi kuhusu wachezaji wa timu yake, yanawekwa hadharani na kampuni moja ya televisheni nchini Ufaransa.
Mourinho amesema alikuwa anatania alipokuwa akilalamika kuwa Chelsea inakosa wachezaji wa nafasi ya ushambuliaji na alimtania Eto'o kuhusu umri wake.
"Yalikuwa mazungumzo ya utani na mtu ambaye hahusiki na masuala ya ulimwengu wa soka," amesema Mourinho.
"Ni fedheha kwa mtu kurekodi mazungumzo binafsi."

Wednesday, February 26, 2014

Miili 5 yapatikana mgodini A. Kusini

Wachimba migodi waliookolewa wiki jana wanakabiliwa na kesi mahakamani ... thumbnail 1 summary

Wachimba migodi waliookolewa wiki jana wanakabiliwa na kesi mahakamani
Miili ya wachimba migodi haramu watano, imepatikana karibu na mgodi ambao ulikuwa hautumiki nchini Afrika Kusini.
Miili ya wanaume wanne na mwanamke mmoja ilipatikana karibu na mgodi huo katika eneo la Roodepoort, Magharibi mwa Johannesburg.
Vifo vyao vimetokea wiki moja baada ya shughuli kubwa ya uokozi wa zaidi ya wachimba migodi 20 haramu waliokuwa wamekwama ndani ya mgodi Mashariki mwa Johannesburg.
Walikamatwa baada ya kuokolewa na sasa wanakabiliwa na kosa la uchimbaji haramu wa migodi.
Afrika Kusini hupoteza mamilioni ya dola katika shughuli za uchimbaji haramu wa madini kila mwaka.
Ardhi inayozingira mji wa Johannesburg ina migodi mingi ambayo haitumiki na ambayo huvutia wachimba migodi haramu kutoka katika eneo hilo na nchi jirani za ,Lesotho, Msumbiji na Zimbabwe.
Mvuto wake hasa huwa ni kwamba zinaweza kuwa na madini ya dhahabu.
Wakati nyingi ya migodi hizo hazina faida za kifedha, bado zina mabaki ya dhahabu kiasi cha kuwavutia watu wengi wasio na ajira.
Waokozi wanasema kuwa bado huenda kuna wachimba migodi haramu zaidi ndani ya migodi hiyo.

Uganda yahofia kunyimwa misaada

Sheria mpya dhidi ya ushoga inatoa adahabu ya maisha jela Waziri wa ... thumbnail 1 summary

Sheria mpya dhidi ya ushoga inatoa adahabu ya maisha jela
Waziri wa mambo ya nje nchini Uganda, Sam Kutesa amesema ana wasiwasi kuwa Marekani huenda ikasitisha msaada wake kwa taifa hilo baada ya Rais Yoweri Museveni kuidhinisha sheria dhidi ya ushoga nchini humo.
Bwana Kutesa amesema kuwa watu sharti wawe na maadili na kukubali msaada.
Balozi wa Marekani nchini Uganda Scott DeLisi, awali aliitaka serikali ya Uganda, kubatilisha sheria hiyo.
Alisema alihitaji kufafanuliwa zaidi sheria hiyo, kabla ya Marekani kujua ikiwa itaendelea na mipango yake ya misaada kwa nchi hiyo hasa miradi ya kupambana dhidi ya HIV na Ukimwi..
Sheria hiyo mpya, inatoa adhabu kali kwa watu wanaoshiriki mapenzi ya jinsia moja na kupiga marufuku kile inachosema kusambaza vitendo vya ushoga.

Ufafanuzi Yakinifu Kutoka Baraza la Mitihani Kuhusu Matokeo ya Kidato Cha nne

UFAFANUZI WA MASWALI MBALIMBALI YA WADAU WA ELIMU KUHUSU MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2013 B... thumbnail 1 summary

UFAFANUZI WA MASWALI MBALIMBALI YA WADAU WA ELIMU KUHUSU MATOKEO YA MTIHANI WA KIDATO CHA NNE (CSEE) 2013

Baraza la Mitihani la Tanzania lilitangaza matokeo ya Mtihani wa Kidato cha Nne (CSEE) 2013 tarehe 21/02/2014. Baada ya kutangazwa kwa matokeo hayo, Baraza limekuwa