Sunday, June 9, 2013

Kala Jeremiah, Ommy Dimpoz, Diamond & Chalz Baba watesa KTMA. List ya washindi wote

Ommy Dimpoz akichukua tuzo ya Video Bora ya Mwaka kwa music vide ya wimbo wa “Baadae” Ben Pol alipochukua tuzo ya Mtunzi Bora wa Mash... thumbnail 1 summary



Ommy Dimpoz akichukua tuzo ya Video Bora ya Mwaka kwa music vide ya wimbo wa "Baadae" Ommy Dimpoz akichukua tuzo ya Video Bora ya Mwaka kwa music vide ya wimbo wa “Baadae”
Ben Pol alipochukua tuzo ya Mtunzi Bora wa Mashahiri Bongo Fleva. Ben Pol alipochukua tuzo ya Mtunzi Bora wa Mashahiri Bongo Fleva.
Msanii wa Bongo Flava kutoka Mwanza, Kala Jeremiah aliibuka na tuzo tatu za Kili Music Awards (KTMA 2013) zilizofanyika jana usiku.  Kala alishinda tuzo ya wimbo bora wa mwaka  (Dear God) na pia aliibuka na tuzo ya msanii bora wa Hip Hop kwa kuwabwaga Fid Q, Joh Makini, Profesa Jay na Stamina waliokua pia nominees kwenye tuzo hiyo.
Advertisement
Ommy Dimpoz naye alishinda  tuzo tatu. Ommy alitwaa tuzo mbili kwa kupitia nyimbo ya “Me and You” aliyofanya collabo na Vanessa Mdee; wimbo bora wa Bongo Pop,  na wimbo bora wa kushirikiana/Kushirikishwa. Ommy alichukua tuzo ya tatu ya video bora ya mwaka kwa kupitia nyimbo ya “Baadae.”
Msanii Diamond Platnumz, ambaye hakuhudhuria tuzo hizo, alishinda moja ya tuzo kubwa usiku huo ya msanii bora wa kiume kwa kuwabwaga Ben Pol, Linex, Mzee Yusuf na Ommy Dimpoz ,na pia alishinda tuzo ya Msanii bora wa kiume Bongo Flava.
Tuzo za muziki wa dance zilitawaliwa na Chalz Baba wa Mashujaa Band aliyeibuka tuzo mbili za Msanii bora wa kiume Bendi na Mtunzi bora wa mashairi – Bendi.
Ifuatayo ni list kamili ya tuzo hizo.
Wimbo bora wa mwaka
Dear God – Kala Jeremiah
Msanii bora wa Kiume
Diamond
Msanii bora wa kike
Lady Jaydee
Msanii bora wa kike Taarab
Isha Mashauzi
Msanii bora wa kiume Taarab
Mzee Yusuf
Msanii bora wa kiume Bongo Flava
Diamond
Msanii bora wa kike Bongo Flava
Recho
Msanii bora wa Hip Hop
Kala Jeremiah
Msanii bora wa kiume Bendi
Chalz Baba
Msanii bora wa kike Bendi
Luiza Mbutu
Msanii bora anayechipukia
Ally Nipishe
Video bora ya mwaka
Baadaye – Ommy Dimpoz
Mtunzi bora wa mashairi Taarab
Mzee Yusuf
Mtunzi bora wa mashairi Bongo Flava
Ben Pol
Mtunzi bora wa mashairi hip hop
Kala Jeremiah
Mtunzi bora wa mashairi Bendi
Chalz Baba
Mtayarishaji bora wa mashairi muziki wa kizazi kipya
Man Walter
Mtayarishaji wa wimbo wa mwaka – Taarab
Enrico
Mtayarishaji wa wimbo mwaka – Bendi
Amoroso
Mtayarishaji chipukizi wa mwaka
Mesen Selekta
Rapper bora wa bendi
Fagasoni
Wimbo bora wenye vionjo vya asili
Chocheeni Kuni – Mrisho Mpoto ft Ditto
Wimbo bora wa bendi
Risasi Kidole – Mashujaa Band
Wimbo bora wa Reggae
Kilimanjaro – Warriors from The East
Wimbo bora wa Afrika Mashariki
Valu Valu – Jose Chameleone
Wimbo bora wa Bongo Pop
Me an You – Ommy Dimpoz ft Vanessa Mdee
Wimbo bora wa kushirikiana/Kushirikishwa
Me and You – Ommy Dimpoz ft Vanessa Mdee
Wimbo bora wa Hip Hop
Nasema Nao – Nay wa Mitego
Wimbo bora wa rnb
Kuwa na Subira – Rama Dee ft. Mapacha
Wimbo bora wa ragga/ dancehall
Predator – Dabo
Wimbo bora wa Taarab
Mjini Chuo Kikuu – Khadija Kopa
Wimbo bora wa zouk rhumba
Ni wewe – Amini
Bendi bora ya mwaka
Mashujaa Band
Kikundi bora cha Taarab
Jahazi Modern Taarab
Kikundi bora cha muziki wa Kizazi kipya
Jambo Squad
Hall of Fame – Institution
Kilimanjaro Band wana Njenje
Hall of Fame – Individual
Salum Abdallah