Tuesday, June 11, 2013

Muigizaji wa filamu nchini, Jaji Khamis (Kashi) afariki dunia leo mchana

Msanii wa filamu nchini Jaji Khamis (Kashi) aliyewahi kutamba na michezo ya ITV enzi zile akiwa na wasanii kama mzee Masinde, Samson na... thumbnail 1 summary

kash-jaji-khamis
Msanii wa filamu nchini Jaji Khamis (Kashi) aliyewahi kutamba na michezo ya ITV enzi zile akiwa na wasanii kama mzee Masinde, Samson na wengine katika mchezo wa Tamu chungu na mingine mingi Amefariki dunia mchana huu katika hosptali ya taifa ya muhimbili alikokuwa amelazwa.

Taarifa za awali zinasema kuwa alikuwa amelazwa hapo kwa muda kiasi kabla ya kufikwa na mauti hayo.

Kwa mujibu wa matandao wa Bongo5, muigizaji mwenzie, Monalisa amethibitisha kifo cha Kashi. Aliongeza kuwa alipata taarifa kwamba Kashi amelazwa Muhimbili akiwa amezidiwa kiasi ha kushindwa kuongea. Monalisa amesema hajajua ni nini kilikua kinamsumbua marehemu Kashi. Msanii Hemedi PHD naye ame-tweet kuhusu taarifa za msiba huo.